< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Ein song, ein salme; av Korahs born. Stor er Herren og høglova i vår Guds by, på hans heilage fjell.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Fager i si høgd, ein fagnad for all jordi er Sions fjell, utkanten av nordheimen, staden til den store kongen.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Gud er i hans hallar kjend som ei fast borg.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
For sjå, kongarne kom saman og drog fram i lag.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Dei såg - so vart dei forfærde, dei vart vitskræmde, flydde i bråhast.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Ein skjelv greip deim der, ei bivring som hjå ei barnsjuk kvinna.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Med austanvind bryt du sund Tarsis-skip.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Liksom me hev høyrt, so hev me no set det i Herren, allhers drotts by, i vår Guds by, Gud gjer honom fast til æveleg tid. (Sela)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Me grundar på din nåde, Gud, midt i ditt tempel.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Som ditt namn, Gud, so er din pris alt til endarne av jordi; di høgre hand er full av rettferd.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Sionsfjellet gled seg, Juda døtter fagnar seg yver dine domar.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Gakk ikring Sion, far rundt um henne, tel hennar tårn!
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Legg merke til hennar vollar, gakk igjenom hennar hallar, so de kann fortelja um det til den komande ætt.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
For denne Gud er vår Gud æveleg og alltid; han skal føra oss ut yver dauden.