< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
En sang, en salme; av Korahs barn. Stor er Herren og høilovet i vår Guds stad, på hans hellige berg.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Fagert hever det sig, en glede for all jorden er Sions berg, det ytterste Norden, den store konges stad.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Gud er i dens borger, han er blitt kjent som et fast vern.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
For se, kongene samlet sig, de drog frem tilsammen.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
De så, da blev de forferdet; de blev slått med redsel, flyktet i hast.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Beven grep dem der, angst som hos en fødende kvinne.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Ved østenvind knuste du Tarsis-skib.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Likesom vi hadde hørt, så har vi nu sett det i Herrens, hærskarenes Guds stad, i vår Guds stad; Gud gjør den fast til evig tid. (Sela)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Vi grunder, Gud, på din miskunnhet midt i ditt tempel.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Som ditt navn, Gud, så er din pris inntil jordens ender; din høire hånd er full av rettferdighet.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Sions berg gleder sig, Judas døtre fryder sig for dine dommers skyld.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Gå omkring Sion og vandre rundt om det, tell dets tårn!
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Gi akt på dets voller, vandre gjennem dets borger, forat I kan fortelle derom til den kommende slekt.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
For denne Gud er vår Gud evindelig og alltid; han skal føre oss ut over døden.