< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Cantico di Salmo, de' figliuoli di Core IL Signore [è] grande, e molto glorioso Nella Città dell'Iddio nostro, [nel] monte della sua santità.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Il monte di Sion, il fondo verso il Settentrione, La Città del gran Re [È in] bella contrada, [è] la gioia di tutta la terra.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Iddio [è] riconosciuto ne' palazzi di essa, per alta fortezza.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Perciocchè ecco, i re si erano adunati, Ed erano tutti insieme passati oltre.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Come prima [la] videro, furono attoniti, Si smarrirono, si affrettarono [a fuggire].
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Tremore li colse quivi; Doglia, come di donna che partorisce.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
[Furono rotti come] per lo vento orientale [Che] rompe le navi di Tarsis.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Come avevamo udito, così abbiam veduto, Nella Città del Signor degli eserciti, Nella Città dell'Iddio nostro; Iddio la stabilirà in perpetuo. (Sela)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
O Dio, noi abbiamo, chetamente aspettata la tua benignità Dentro al tuo Tempio.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
O Dio, quale [è] il tuo Nome, Tale [è] la tua lode, infino all'estremità della terra; La tua destra è piena di giustizia.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Il monte di Sion si rallegrerà, Le figliuole di Giuda festeggeranno, per li tuoi giudicii.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Circuite Sion, e andate attorno a lei, Contate le sue torri.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Ponete mente alle bastie, Mirate l'altezza de' suoi palazzi; Acciocchè [lo] raccontiate all'età a venire.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Perciocchè questo Dio [è] il nostro Dio in sempiterno; Egli ci giuderà infino alla morte.