< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Nyanyian. Mazmur bani Korah. Besarlah TUHAN dan sangat terpuji di kota Allah kita!
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Gunung-Nya yang kudus, yang menjulang permai, adalah kegirangan bagi seluruh bumi; gunung Sion itu, jauh di sebelah utara, kota Raja Besar.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Dalam puri-purinya Allah memperkenalkan diri-Nya sebagai benteng.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Sebab lihat, raja-raja datang berkumpul, mereka bersama-sama berjalan maju;
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
demi mereka melihatnya, mereka tercengang-cengang, terkejut, lalu lari kebingungan.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Kegentaran menimpa mereka di sana; mereka kesakitan seperti perempuan yang hendak melahirkan.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Dengan angin timur Engkau memecahkan kapal-kapal Tarsis.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Seperti yang telah kita dengar, demikianlah juga kita lihat, di kota TUHAN semesta alam, di kota Allah kita; Allah menegakkannya untuk selama-lamanya. (Sela)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Kami mengingat, ya Allah, kasih setia-Mu di dalam bait-Mu.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Seperti nama-Mu, ya Allah, demikianlah kemasyhuran-Mu sampai ke ujung bumi; tangan kanan-Mu penuh dengan keadilan.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Biarlah gunung Sion bersukacita; biarlah anak-anak perempuan Yehuda bersorak-sorak oleh karena penghukuman-Mu!
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Kelilingilah Sion dan edarilah dia, hitunglah menaranya,
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
perhatikanlah temboknya, jalanilah puri-purinya, supaya kamu dapat menceriterakannya kepada angkatan yang kemudian:
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Sesungguhnya inilah Allah, Allah kitalah Dia seterusnya dan untuk selamanya! Dialah yang memimpin kita!

< Zaburi 48 >