< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
שיר מזמור לבני-קרח ב גדול יהוה ומהלל מאד-- בעיר אלהינו הר-קדשו
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
יפה נוף משוש כל-הארץ הר-ציון ירכתי צפון קרית מלך רב
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
אלהים בארמנותיה נודע למשגב
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
כי-הנה המלכים נועדו עברו יחדו
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
המה ראו כן תמהו נבהלו נחפזו
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
רעדה אחזתם שם חיל כיולדה
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
ברוח קדים-- תשבר אניות תרשיש
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
כאשר שמענו כן ראינו-- בעיר-יהוה צבאות בעיר אלהינו אלהים יכוננה עד-עולם סלה
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
דמינו אלהים חסדך-- בקרב היכלך
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
כשמך אלהים-- כן תהלתך על-קצוי-ארץ צדק מלאה ימינך
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
ישמח הר ציון--תגלנה בנות יהודה למען משפטיך
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
סבו ציון והקיפוה ספרו מגדליה
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
שיתו לבכם לחילה--פסגו ארמנותיה למען תספרו לדור אחרון
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
כי זה אלהים אלהינו--עולם ועד הוא ינהגנו על-מות

< Zaburi 48 >