< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Ein Lied, ein Psalm für die Söhne Korachs. Groß ist Jehovah, und sehr zu loben in unseres Gottes Stadt, auf dem Berge Seiner Heiligkeit.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Schön erstreckt sich der ganzen Erde Freude, der Berg Zion von den Seiten der Mitternacht, die Stadt des großen Königs.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Gott ist in ihren Palästen bekannt als Burg.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Denn siehe, die Könige taten sich zusammen, sie gingen allesamt vorüber.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Sie sahen, so staunten sie, sie waren bestürzt, sie enteilten.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Beben ergriff sie da, ein Kreißen wie die Gebärerin.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Durch den Ostwind zerbrichst Du die Schiffe von Tharschisch.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Wie wir es gehört hatten, so sahen wir es in der Stadt Jehovahs der Heerscharen, in unseres Gottes Stadt; Gott festigt sie ewiglich. (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Gott, wir bedenken Deine Barmherzigkeit inmitten Deines Tempels.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Wie Dein Name, o Gott, so ist Dein Lob bis an die Enden der Erde. Voller Gerechtigkeit ist Deine Rechte.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Es sei fröhlich der Berg Zion, frohlocken sollen Judahs Töchter um Deiner Gerichte willen.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Ziehet um Zion, umringet es, zählt seine Türme.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Und richtet euer Herz auf seine Vormauer, durchforscht seine Paläste, daß ihr es einem späteren Geschlechte erzählt,
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Daß dieser Gott ist unser Gott ewig und immerfort, Er geleitet uns bis zum Tode.

< Zaburi 48 >