< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Psaume du cantique aux fils de Coré pour le second jour de la semaine. Le Seigneur est grand et très digne de louange, dans la cité de notre Dieu, et sur sa montagne sainte.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
La montagne de Sion est fondée à l’exultation de toute la terre; du côté de l’aquilon est la cité du grand Roi.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Dieu sera connu dans ses maisons, quand il en prendra la défense.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Car voilà que les rois de la terre se sont réunis et sont venus ensemble.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
L’ayant vu eux-mêmes, ils ont été étonnés, ils ont été troublés, ils ont été fort émus:
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Un tremblement les a saisis. Là ils ont ressenti comme les douleurs d’une femme qui enfante:
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Ainsi par un vent impétueux, vous briserez les vaisseaux de Tharsis.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Ce que nous avions appris, nous l’avons vu dans la cité du Seigneur des armées, dans la cité de notre Dieu: Dieu l’a fondée pour l’éternité.
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Nous avons reçu, ô Dieu, votre miséricorde, au milieu de votre temple.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Comme votre nom, ô Dieu, ainsi votre louange s’étend jusqu’aux extrémités de la terre: votre droite est pleine de justice.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Que la montagne de Sion se réjouisse, et que les filles de Juda tressaillent d’allégresse, à cause de vos jugements, Seigneur.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Environnez Sion et embrassez-la: racontez toutes ces choses dans ses tours.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Portez votre attention sur sa force: faites le dénombrement de ses maisons, afin que vous le racontiez à une autre génération.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Parce que c’est lui qui est Dieu, notre Dieu pour l’éternité et pour les siècles des siècles: lui-même qui nous gouvernera dans les siècles.

< Zaburi 48 >