< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Cantique des fils de Coré. L'Éternel est grand et digne d'être loué, dans la cité de notre Dieu, sur sa montagne sainte.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Délices de toute la terre, le mont de Sion s'élève magnifique, sur ses flancs au Nord il porte la ville du grand Roi.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Dieu pour ses palais s'est montré un rempart.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Car voici, les rois se liguèrent: ensemble ils disparurent.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Ils virent, et furent aussitôt éperdus, ils prirent l'épouvante, et s'enfuirent;
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
là même ils furent saisis du tremblement, des angoisses de l'enfantement,
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
au souffle du vent d'Orient, qui fracasse les navires de Tarsis.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Ce qu'on nous avait dit, nous l'avons vu nous-mêmes dans la ville de l'Éternel des armées, ville de notre Dieu; Dieu la maintient à jamais. (Pause)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
O Dieu, nous pensons à ta grâce dans l'enceinte de ton temple.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Que ta louange, ô Dieu, aussi bien que ton nom, retentisse jusqu'aux bouts de la terre! De justice ta droite est remplie.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
La montagne de Sion est dans la joie, et les filles de Juda dans l'allégresse, à cause de tes jugements.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Faites le tour de Sion et de son enceinte, comptez ses tours,
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
examinez son fossé, faites la revue de ses palais, pour en parler à la race future!
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Car ce Dieu est notre Dieu pour toujours, à jamais: Il nous conduira jusqu'à la mort.

< Zaburi 48 >