< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Psaume chanté par les fils de Koré, le second jour de la semaine. Le Seigneur est grand et digne de toute louange en la ville de notre Dieu, sur sa montagne sainte.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Elle est profondément enracinée aux cris de joie de toute la terre, la montagne de Sion; la ville du grand Roi est bâtie sur le côté qui regarde l'aquilon.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Dieu est connu dans ses palais, lorsqu'il la défend,
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Car voilà que les rois de la terre se sont rassemblés; ils sont venus en un même lieu.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Mais l'ayant vu, ils ont été si émerveillés, qu'ils se sont troublés et ont été ébranlés.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
L'effroi les a saisis, et ils ont éprouvé comme les douleurs de l'enfantement.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
D'un coup de vent impétueux tu briseras les vaisseaux de Tharsis.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Ce que nous avions ouï, ainsi nous l'avons vu en la ville du Seigneur des armées, en la cité de notre Dieu. Dieu l'a fondée pour toujours. (Pause)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
O Dieu, nous avons reçu ta miséricorde au milieu de ton temple.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Comme ton nom, ô Dieu, ta louange va jusqu'aux confins de la terre; ta droite est pleine de justice.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Que la montagne de Sion se réjouisse; que les villes de Juda tressaillent à cause de tes jugements, ô Seigneur!
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Entourez Sion, embrassez-la; discourez au sujet de ses tours.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Mettez vos cœurs dans sa force, et distribuez ses demeures, afin que vous racontiez ces choses à une autre génération.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Car c'est notre Dieu dans le siècle présent et dans tous les siècles à venir; et il sera notre pasteur dans tous les siècles.

< Zaburi 48 >