< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Cantique. Psaume des fils de Coré. L’Éternel est grand et fort digne de louange dans la ville de notre Dieu, dans sa montagne sainte.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Belle dans son élévation, la joie de toute la terre, est la montagne de Sion, aux côtés du nord, la ville du grand roi;
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Dieu est connu dans ses palais pour une haute retraite.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Car voici, les rois se sont assemblés, ils ont passé outre ensemble:
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Ils ont vu, – ils ont été étonnés; ils ont été troublés, ils se sont enfuis consternés.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Là, le tremblement les a saisis, une angoisse comme [celle de] la femme qui enfante.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Par le vent d’orient tu as brisé les navires de Tarsis.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Comme nous avons entendu, ainsi nous l’avons vu dans la ville de l’Éternel des armées, dans la ville de notre Dieu: Dieu l’établit pour toujours. (Sélah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Ô Dieu! nous avons pensé à ta bonté, au milieu de ton temple.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Ô Dieu! comme ton nom, ainsi est ta louange, jusqu’aux bouts de la terre; ta droite est pleine de justice.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Que la montagne de Sion se réjouisse, que les filles de Juda s’égaient, à cause de tes jugements.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Faites le tour de Sion, et faites-en le circuit; comptez ses tours,
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Faites attention à son rempart, considérez ses palais, afin que vous le racontiez à la génération à venir.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Car ce Dieu est notre Dieu, pour toujours et à perpétuité; il sera notre guide jusqu’à la mort.

< Zaburi 48 >