< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
A Song [and] Psalm for the sons of Korah. Great [is] the LORD, and greatly to be praised in the city of our God, [in] the mountain of his holiness.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Beautiful for situation, the joy of the whole earth, [is] mount Zion, [on] the sides of the north, the city of the great King.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
God is known in her palaces for a refuge.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
For lo, the kings were assembled, they passed by together.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
They saw [it], [and] so they wondered; they were troubled, [and] hasted away.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Fear took hold upon them there, [and] pain, as of a woman in travail.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Thou breakest the ships of Tarshish with an east wind.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
As we have heard, so have we seen in the city of the LORD of hosts, in the city of our God: God will establish it for ever. (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
We have thought of thy loving-kindness, O God, in the midst of thy temple.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
According to thy name, O God, so [is] thy praise to the ends of the earth: thy right hand is full of righteousness.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Let mount Zion rejoice, let the daughters of Judah be glad, because of thy judgments.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Walk about Zion, and go round her: number her towers.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Mark ye well her bulwarks, consider her palaces; that ye may tell [it] to the generation following.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
For this God [is] our God for ever and ever: he will be our guide [even] to death.

< Zaburi 48 >