< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
song melody to/for son: descendant/people Korah great: large LORD and to boast: praise much in/on/with city God our mountain: mount holiness his
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
beautiful elevation rejoicing all [the] land: country/planet mountain: mount Zion flank Zaphon town king many
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
God in/on/with citadel: palace her to know to/for high refuge
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
for behold [the] king to appoint to pass together
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
they(masc.) to see: see so to astounded to dismay to hurry
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
trembling to grasp them there agony like/as to beget
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
in/on/with spirit: breath east to break fleet Tarshish
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
like/as as which to hear: hear so to see: see in/on/with city LORD Hosts in/on/with city God our God to establish: establish her till forever: enduring (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
to resemble God kindness your in/on/with entrails: among temple your
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
like/as name your God so praise your upon boundary land: country/planet righteousness to fill right your
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
to rejoice mountain: mount Zion to rejoice daughter Judah because justice: judgement your
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
to turn: surround Zion and to surround her to recount tower her
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
to set: consider heart your to/for bulwark her to go through citadel: palace her because to recount to/for generation last
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
for this God God our forever: enduring and perpetuity he/she/it to lead us upon to die

< Zaburi 48 >