< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
A song a psalm of [the] sons of Korah. [is] great Yahweh and [is] to be praised exceedingly in [the] city of God our [the] mountain of holiness his.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
[it is] beautiful of Height [the] joy of all the earth [the] mountain of Zion [the] remotest parts of Zaphon [the] town of [the] king great.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
God [is] in fortresses its he has made himself known to a refuge.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
For there! the kings they assembled they passed on together.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
They they saw thus they were astonished they were terrified they hurried away.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Trembling it seized them there anguish like [woman] giving birth.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
With a wind of [the] east you shatter ships of Tarshish.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Just as we have heard - so we have seen in [the] city of Yahweh of hosts in [the] city of God our God he will establish it until perpetuity (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
We have reflected on O God covenant loyalty your in [the] midst of temple your.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Like name your O God so praise your [is] over [the] ends of [the] earth righteousness it is full right [hand] your.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
It will rejoice - [the] mountain of Zion they will be glad [the] daughters of Judah on account of judgments your.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Go around Zion and go round it count towers its.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Set heart your - to rampart its walk through fortresses its so that you may recount [it] to a generation later.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
For this - [is] God God our forever and ever he he will guide us on dying.