< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
“A psalm of the sons of Korah.” Great is Jehovah, and greatly to be praised In the city of our God, upon his holy mountain.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Beautiful in its elevation is Mount Zion, The joy of the whole earth; The joy of the farthest North is the city of the great king;
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
In her palaces God is known as a refuge.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
For, lo! kings were assembled against it; They passed away together.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
As soon as they saw, they were astonished; They were confounded, and hasted away.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
There terror seized upon them, —Pain, as of a woman in travail;
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
As when the east wind breaketh in pieces The ships of Tarshish.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
As we have heard, so have we seen In the city of the LORD of hosts, in the city of our God; God will establish it for ever. (Pause)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
We think of thy loving-kindness, O God! In the midst of thy temple!
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
As thy name, O God! so thy praise, extendeth to the ends of the earth; Thy right hand is full of righteousness.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Mount Zion rejoiceth, The daughters of Judah exult, On account of thy righteous judgments.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Go round about Zion; number her towers;
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Mark well her bulwarks; count her palaces; That ye may tell it to the next generation!
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
For this God is our God for ever and ever; He will be our guide unto death.