< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
“A song and psalm by the sons of Korach.” Great is the Lord, and highly praised in the city of our God, [in] his holy mountain.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
A beautiful district, the joy of the whole earth, is mount Zion, the farthest north, the city of the great King.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
God is become known in her palaces as a defence.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
For, lo, the kings were assembled, they are passed away together.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
They indeed saw—[and] so they were astonished; they were terrified, they were confounded.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Trembling seized on them there, pain, as on a woman in travail.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
With the east wind thou breakest the ships of Tharshish.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
As we have heard, so have we seen [it] in the city of the Lord of hosts, in the city of our God: God will establish it for ever. (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
We have reflected on thy kindness, O God, in the midst of thy temple.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
As thy name is, O God, so is thy praise over the ends of the earth: of righteousness is thy right hand full.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Let mount Zion rejoice, let the daughters of Judah be glad, because of thy judgments.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Compass Zion about, and walk round about her; number her towers.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Direct your mind to her outer wall, mark carefully her palaces: in order that ye may tell it to the latest generation.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
For this One is God, our God for ever and ever: he will be our guide even unto death.