< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
A Song. A Psalm. Of the sons of Korah. Great is the Lord and greatly to be praised, in the town of our God, in his holy mountain.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Beautiful in its high position, the joy of all the earth, is the mountain of Zion, the mountain of God, the town of the great King.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
In its buildings God is seen to be a high tower.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
For see! the kings came together by agreement, they were joined together.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
They saw it, and so were full of wonder; they were troubled, and went quickly away in fear.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Shaking came on them and pain, as on a woman in childbirth.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
By you the ships of Tarshish are broken as by an east wind.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
As it came to our ears so have we seen it, in the town of the Lord of armies, in the town of our God; God will keep it fixed for ever. (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Our thoughts were of your mercy, O God, while we were in your Temple.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
As your name is, O God, so is your praise to the ends of the earth; your right hand is full of righteousness.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Let there be joy in the mountain of Zion, and let the daughters of Judah be glad, because of your wise decisions.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Make your way about Zion, and go round it, numbering its towers.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Take note of its strong walls, looking well at its fair buildings; so that you may give word of it to the generation which comes after.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Because this God is our God for ever and ever: he will be our guide.