< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
(En sang. En salme af Koras sønner.) Stor og højlovet er vor Gud i sin Stad.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Smukt løfter sig hans hellige Bjerg, al Jordens Fryd, Zions Bjerg i det højeste Nord, den store Konges By.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Som Værn gjorde Gud sig kendt i dens Borge.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Thi Kongerne samlede sig, rykked frem tilsammen;
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
de så og tav på Stedet, flyed i Angst,
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
af Rædsel grebes de brat, af Veer som en, der føder.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Med Østenstormen knuser du Tarsisskibe.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Som vi havde hørt det, så vi det selv i Hærskarers HERREs By, i vor Guds By; til evig Tid lader Gud den stå. (Sela)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
I din Helligdom tænker vi, Gud, på din Miskundhed;
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
som dit Navn så lyder din Pris til Jordens Grænser. Din højre er fuld af Retfærd,
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Zions Bjerg fryder sig, Judas Døtre jubler over dine Domme.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Drag rundt om Zion, gå rundt og tæl dets Tårne,
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
læg Mærke til dets Ringmur, så gennem dets Borge, at I kan melde Slægten, der
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
kommer: Sådan er Gud, vor Gud for evigt og altid, han skal lede os.

< Zaburi 48 >