< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
En Sang. En Salme af Koras Sønner.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Stor og højlovet er vor Gud i sin Stad.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Smukt løfter sig hans hellige Bjerg, al Jordens Fryd, Zions Bjerg i det højeste Nord, den store Konges By.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Som Værn gjorde Gud sig kendt i dens Borge.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Thi Kongerne samlede sig, rykked frem tilsammen;
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
de saa og tav paa Stedet, flyed i Angst,
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
af Rædsel grebes de brat, af Veer som en, der føder.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Med Østenstormen knuser du Tarsisskibe.
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Som vi havde hørt det, saa vi det selv i Hærskarers HERRES By, i vor Guds By; til evig Tid lader Gud den staa. (Sela)
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
I din Helligdom tænker vi, Gud, paa din Miskundhed;
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
som dit Navn saa lyder din Pris til Jordens Grænser. Din højre er fuld af Retfærd,
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Zions Bjerg fryder sig, Judas Døtre jubler over dine Domme.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Drag rundt om Zion, gaa rundt og tæl dets Taarne,
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
læg Mærke til dets Ringmur, gaa gennem dets Borge, at I kan melde Slægten, der kommer: Saadan er Gud, vor Gud for evigt og altid, han skal lede os. Al-mut.