< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Píseň žalmu synů Chóre. Veliký jest Hospodin, a převelmi chvalitebný v městě Boha našeho, na hoře svatosti své.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Ozdoba krajiny, útěcha vší země jestiť hora Sion, k straně půlnoční, město krále velikého.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Bůh na palácích jeho, a znají ho býti vysokým hradem.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Nebo aj, králové když se shromáždili a spolu táhli,
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Sami to uzřevše, velmi se divili, a předěšeni byvše, náhle utíkali.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Tuť jest je strach popadl, a bolest jako ženu rodící.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Větrem východním rozrážíš lodí Tarské.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Jakž jsme slýchali, tak jsme spatřili, v městě Hospodina zástupů, v městě Boha našeho. Bůh upevní je až na věky.
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Rozjímáme, ó Bože, milosrdenství tvé u prostřed chrámu tvého.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Jakož jméno tvé, Bože, tak i chvála tvá až do končin země; pravice tvá zajisté plná jest spravedlnosti.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Raduj se, horo Sione, plésejte, dcery Judské, z příčiny soudů Božích.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Obejděte Sion, a obstupte jej, sečtěte věže jeho.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Přiložte mysl svou k ohradě, popatřte na paláce jeho, abyste uměli vypravovati věku potomnímu,
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Že tento Bůh jest Bůh náš na věčné věky, a že on vůdce náš bude až do smrti.