< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
可拉後裔的詩歌。 耶和華本為大! 在我們上帝的城中, 在他的聖山上,該受大讚美。
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
錫安山-大君王的城, 在北面居高華美, 為全地所喜悅。
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
上帝在其宮中, 自顯為避難所。
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
看哪,眾王會合, 一同經過。
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
他們見了這城就驚奇喪膽, 急忙逃跑。
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
他們在那裏被戰兢疼痛抓住, 好像產難的婦人一樣。
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
上帝啊,你用東風打破他施的船隻。
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
我們在萬軍之耶和華的城中 -就是我們上帝的城中-所看見的, 正如我們所聽見的。 上帝必堅立這城,直到永遠。 (細拉)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
上帝啊,我們在你的殿中想念你的慈愛。
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
上帝啊,你受的讚美正與你的名相稱,直到地極! 你的右手滿了公義。
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
因你的判斷,錫安山應當歡喜, 猶大的城邑應當快樂。
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
你們當周遊錫安, 四圍旋繞,數點城樓,
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
細看她的外郭, 察看她的宮殿, 為要傳說到後代。
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
因為這上帝永永遠遠為我們的上帝; 他必作我們引路的,直到死時。

< Zaburi 48 >