< Zaburi 47 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Pigeni makofi, enyi mataifa yote, mpigieni Mungu kelele za shangwe!
Al la ĥorestro. De la Koraĥidoj. Psalmo. Ĉiuj popoloj, plaŭdu per la manoj, Kriu al Dio per voĉo de kanto.
2 Jinsi gani alivyo wa kutisha, Bwana Aliye Juu Sana, Mfalme mkuu juu ya dunia yote!
Ĉar la Eternulo Plejalta estas timinda; Li estas granda Reĝo super la tuta tero.
3 Ametiisha mataifa chini yetu watu wengi chini ya miguu yetu.
Li subigas al ni popolojn Kaj metas gentojn sub niajn piedojn.
4 Alituchagulia urithi wetu, fahari ya Yakobo, aliyempenda.
Li elektas por ni nian heredon, La majeston de Jakob, kiun Li amas. (Sela)
5 Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti za tarumbeta.
Dio supreniras ĉe sonoj de ĝojo, La Eternulo ĉe trumpetado.
6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa, mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.
Kantu al Dio, kantu! Kantu al nia Reĝo, kantu!
7 Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote, mwimbieni zaburi za sifa.
Ĉar Dio estas la Reĝo de la tuta tero: Kantu edifan kanton!
8 Mungu anatawala juu ya mataifa, Mungu ameketi juu ya kiti chake cha enzi kitakatifu.
Dio reĝas super la popoloj; Dio sidas sur Sia sankta trono.
9 Wakuu wa mataifa wanakusanyika kama watu wa Mungu wa Abrahamu, kwa kuwa wafalme wa dunia ni mali ya Mungu; yeye ametukuka sana.
La princoj de la popoloj kolektiĝis, La popolo de la Dio de Abraham; Ĉar al Dio apartenas la ŝildoj de la tero; Li estas tre alta.