< Zaburi 46 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Al maestro del coro. Dei figli di Core. Su «Le vergini...». Canto. Dio è per noi rifugio e forza, aiuto sempre vicino nelle angosce.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
Perciò non temiamo se trema la terra, se crollano i monti nel fondo del mare.
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
Fremano, si gonfino le sue acque, tremino i monti per i suoi flutti.
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
Un fiume e i suoi ruscelli rallegrano la città di Dio, la santa dimora dell'Altissimo.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
Dio sta in essa: non potrà vacillare; la soccorrerà Dio, prima del mattino.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
Fremettero le genti, i regni si scossero; egli tuonò, si sgretolò la terra.
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Il Signore degli eserciti è con noi, nostro rifugio è il Dio di Giacobbe.
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Venite, vedete le opere del Signore, egli ha fatto portenti sulla terra.
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
Farà cessare le guerre sino ai confini della terra, romperà gli archi e spezzerà le lance, brucerà con il fuoco gli scudi.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
Fermatevi e sappiate che io sono Dio, eccelso tra le genti, eccelso sulla terra.
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Il Signore degli eserciti è con noi, nostro rifugio è il Dio di Giacobbe.