< Zaburi 46 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Auf den Siegesspender, von den Korachiten, mit verborgenem Sinne ein Gesang. Gott ist uns Schutz und Zuversicht, in Nöten eine Hilfe, leicht zu finden.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
Drum fürchteten wir uns auch nicht, selbst wenn die Erde wankte, versänken Berge gar ins Meer,
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
daß seine Wasser tosend schäumten, daß selbst vor seinem Wüten Berge bebten. (Sela)
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
Ein Strom ist da. Die Gottesstadt erfreuen seine Arme, die heiligste der Wohnungen des Höchsten.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
In ihr ist Gott; sie kann nicht wanken. Gott steht ihr bei noch vor der Morgenwende. -
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
Die Heidenvölker tobten. Reiche wankten. Darein gedonnert hat er, daß die Erde bebte. -
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Der Herr der Heeresscharen ist mit uns; und eine Burg ist Jakobs Gott für uns. (Sela)
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Herbei und schaut des Herrn Taten, der überaus Erstaunliches im Land getan!
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
Die Kämpfe läßt er ruhn bis an des Landes Grenze. zerbricht die Bogen und zerschlägt die Speere, verbrennt die Schilde. -
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
"Laßt ab! Bedenket: Ich bin Gott! Ich will erhaben bei den Heiden sein, wie ich erhaben bin im eignen Lande."
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Der Herr der Heeresscharen ist mit uns; und eine Burg ist Jakobs Gott für uns. (Sela)