< Zaburi 46 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Au maître-chantre. — Des enfants de Coré. — Cantique pour voix de jeunes filles. Dieu est pour nous un refuge, un rempart. Un secours dans nos détresses: On trouve aisément accès auprès de lui.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
C'est pourquoi nous ne craindrons rien, Quand même la terre serait bouleversée, Et que les montagnes seraient ébranlées au sein de la mer,
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
Quand même les flots mugiraient en bouillonnant. Et que leur furie ferait trembler les montagnes. (Pause)
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
Il est un fleuve, dont les flots réjouissent la cité de Dieu, Le sanctuaire de la Demeure du Très-Haut.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
Dieu est au milieu d'elle: elle ne sera point ébranlée. Dieu lui donne son secours dès l'aube du matin.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
Les nations s'agitent, les nations s'ébranlent: Il fait entendre sa voix, et la terre tremble.
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
L'Éternel des armées est avec nous; Le Dieu de Jacob est notre haute retraite. (Pause)
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Venez, contemplez les oeuvres de l'Éternel, Les étonnants prodiges qu'il accomplit sur la terre.
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
Il fait cesser les combats jusqu'aux extrémités du monde; Il rompt les arcs et brise les lances; Il brûle les chars au feu.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
«Arrêtez, dit-il, et sachez que c'est moi qui suis Dieu. Je domine sur les nations, je domine sur la terre!»
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
L'Éternel des armées est avec nous; Le Dieu de Jacob est notre haute retraite. (Pause)

< Zaburi 46 >