< Zaburi 46 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Au chef des chantres. Par les fils de Coré. Cantique sur les Alamoth. Dieu est pour nous un abri, une force, un appui dans les tourments, facilement accessible.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
Aussi ne craindrons-nous rien, dût la terre bouger de sa place, et les montagnes s’abîmer au sein de l’Océan;
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
dussent ses flots gronder et bouillonner, et les montagnes trembler quand il entre en fureur!
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
Le fleuve…! Ses ondes réjouissent la ville de Dieu, demeure sainte du Très-Haut.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
Dieu réside au milieu d’elle: elle ne sera point ébranlée, Dieu venant à son secours dès le lever de l’aurore.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
Les peuples s’agitent, les royaumes chancellent; il fait retentir sa voix: la terre se liquéfie!
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
L’Eternel-Cebaot est avec nous, le Dieu de Jacob est une citadelle pour nous. (Sélah)
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Venez, contemplez les œuvres de l’Eternel, qui a opéré des ruines sur la terre!
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
Il met fin aux guerres jusqu’aux confins du globe, il brise les arcs, met en pièces les lances, et livre au feu les chars des combats.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
Tenez-vous cois et sachez que moi, je suis Dieu, grand parmi les peuples, grand sur la terre!
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
L’Eternel-Cebaot est avec nous, le Dieu de Jacob est une citadelle pour nous. (Sélah)

< Zaburi 46 >