< Zaburi 46 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
“For the leader of the music. Of, or for, the sons of Korah. To be sung in the manner, or with the voice, of virgins.” God is our refuge and strength; An ever present help in trouble.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
Therefore will we not fear, though the earth be changed; Though the mountains tremble in the heart of the sea;
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
Though its waters roar and be troubled, And the mountains shake with the swelling thereof. (Pause)
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
A river with its streams shall make glad the city of God, The holy dwelling-place of the Most High.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
God is the midst of her; she shall not be moved; God will help her, and that full early.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
The nations raged; kingdoms were moved; He uttered his voice, the earth melted.
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The LORD of hosts is with us; The God of Jacob is our refuge. (Pause)
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Come, behold the doings of the LORD; What desolations he hath made in the earth!
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
He causeth wars to cease to the end of the earth; He hath broken the bow, and snapped the spear asunder, And burned the chariots in fire.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
“Desist, and know that I am God; I will be exalted among the nations, I will be exalted throughout the earth!”
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The LORD of hosts is with us; The God of Jacob is our refuge.