< Zaburi 46 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
God is our refuge and strength, a very present help in trouble.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
Therefore will not we fear, though the earth be removed, and though the mountains be carried into the middle of the sea;
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
Though the waters thereof roar and be troubled, though the mountains shake with the swelling thereof. (Selah)
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
There is a river, the streams whereof shall make glad the city of God, the holy place of the tabernacles of the most High.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
God is in the middle of her; she shall not be moved: God shall help her, and that right early.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
The heathen raged, the kingdoms were moved: he uttered his voice, the earth melted.
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The LORD of hosts is with us; the God of Jacob is our refuge. (Selah)
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Come, behold the works of the LORD, what desolations he has made in the earth.
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
He makes wars to cease to the end of the earth; he breaks the bow, and cuts the spear in sunder; he burns the chariot in the fire.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
Be still, and know that I am God: I will be exalted among the heathen, I will be exalted in the earth.
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The LORD of hosts is with us; the God of Jacob is our refuge. (Selah)

< Zaburi 46 >