< Zaburi 46 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
For the music director by the sons of Korah. According to alamoth, a song. God is our protection and our strength; always ready to help when troubles come.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
So we will not be afraid though the earth shakes, though the mountains fall into the depths of the sea,
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
though the waters roar and foam, though the mountains tremble as the waters surge violently! (Selah)
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
A river flows to bring happiness to those in God's city, the holy place where the Most High lives.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
God is in the midst of the city; it will never fall. God protects it as soon as it is light.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
Nations are in turmoil, kingdoms collapse. God raises his voice and the earth melts.
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The Lord Almighty is with us; the God of Jacob protects us. (Selah)
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Come and see what the Lord has achieved! See the amazing things he has done on the earth!
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
He stops wars all over the world. He smashes the bow; he breaks the spear; he sets shields on fire.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
Stop fighting! Recognize I am God! I am the ruler of the nations; I am the ruler of the earth.
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The Lord Almighty is with us; the God of Jacob protects us. (Selah)