< Zaburi 46 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Unto the end. To the sons of Korah, for confidants. A Psalm. Our God is our refuge and strength, a helper in the tribulations that have greatly overwhelmed us.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
Because of this, we will not be afraid when the earth will be turbulent and the mountains will be transferred into the heart of the sea.
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
They thundered, and the waters were stirred up among them; the mountains have been disturbed by his strength.
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
The frenzy of the river rejoices the city of God. The Most High has sanctified his tabernacle.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
God is in its midst; it will not be shaken. God will assist it in the early morning.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
The peoples have been disturbed, and the kingdoms have been bowed down. He uttered his voice: the earth has been moved.
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The Lord of hosts is with us. The God of Jacob is our supporter.
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Draw near and behold the works of the Lord: what portents he has set upon the earth,
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
carrying away wars even to the end of the earth. He will crush the bow and break the weapons, and he will burn the shield with fire.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
Be empty, and see that I am God. I will be exalted among the peoples, and I will be exalted upon the earth.
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The Lord of hosts is with us. The God of Jacob is our supporter.