< Zaburi 46 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
For the Chief Musician. By the sons of Korah. According to Alamoth. God is our refuge and strength, a very present help in trouble.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
Therefore we will not be afraid, though the earth changes, though the mountains are shaken into the heart of the seas;
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
though its waters roar and are troubled, though the mountains tremble with their swelling. (Selah)
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
There is a river, the streams of which make the city of God glad, the holy place of the tents of the Most High.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
God is within her. She shall not be moved. God will help her at dawn.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
The nations raged. The kingdoms were moved. He lifted his voice and the earth melted.
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The LORD of Armies is with us. The God of Jacob is our refuge. (Selah)
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Come, see the LORD’s works, what desolations he has made in the earth.
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
He makes wars cease to the end of the earth. He breaks the bow, and shatters the spear. He burns the chariots in the fire.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
“Be still, and know that I am God. I will be exalted among the nations. I will be exalted in the earth.”
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
The LORD of Armies is with us. The God of Jacob is our refuge. (Selah)

< Zaburi 46 >