< Zaburi 46 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
科辣黑後裔的詩歌,交與樂官,女聲高音。 天主是我們的救助和力量,天主是患難中最易尋到的保障。
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
因此,縱使地動山崩,墮入海心,我們也決不會疑懼橫生;
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
海濤儘管洶湧翻騰,山岳儘管因浪震動:我們同在的是萬軍的天主,雅各伯的天主是我們的保護。
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
河流要使天主的城邑歡樂,即至高者所住的至聖居所,
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
天主定居其中,此城決不動搖;清晨曙光一現,天主即加扶牢。
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
異民儘管擾亂,萬邦儘管騷動,天主一發鳴聲,大地即刻消溶。
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
與我們同在的是萬軍的上主,雅各伯的天主是我們的保護。
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
請你們前來觀看上主的作為,看祂在地上所行的驚人事蹟:
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
祂消滅戰爭直達地極,祂斷弓毀矛,燒甲焚盔。
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
你們要停手!應承認我是天主,是萬民的至尊,是大地的上主。
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
與我們同在的,是萬軍的上主,雅各伯的天主是我們的保護。

< Zaburi 46 >