< Zaburi 45 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
Müzik şefi için - “Zambaklar” makamında Korahoğulları'nın Maskili - Aşk ilahisi Yüreğimden güzel sözler taşıyor, Kral için söylüyorum şiirlerimi, Dilim usta bir yazarın kalemi gibi olsun.
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
Sen insanların en güzelisin, Lütuf saçılmış dudaklarına. Çünkü Tanrı seni sonsuza dek kutsamış.
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
Ey yiğit savaşçı, kuşan kılıcını beline, Görkemine, yüceliğine bürün.
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
At sırtında görkeminle, zaferle ilerle, Gerçek ve adalet uğruna Sağ elin korkunç işler göstersin.
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
Okların sivridir, Kral düşmanlarının yüreğine saplanır, Halklar ayaklarının altına serilir.
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
Ey Tanrı, tahtın sonsuzluklar boyunca kalıcıdır, Krallığının asası adalet asasıdır.
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
Doğruluğu sever, kötülükten nefret edersin. Bunun için Tanrı, senin Tanrın, Seni sevinç yağıyla Arkadaşlarından daha çok meshetti.
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
Giysilerinin tümü mür, öd, tarçın kokuyor; Fildişi saraylardan gelen çalgı sesleri seni eğlendiriyor!
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
Kral kızları senin saygın kadınların arasında, Kraliçe, Ofir altınları içinde senin sağında duruyor.
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Dinle, ey kral kızı, bak, kulak ver, Halkını, baba evini unut.
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
Kral senin güzelliğine vuruldu, Efendin olduğu için önünde eğil.
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
Sur halkı armağan getirecek, Halkın zenginleri lütfunu kazanmak isteyecek.
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
Kral kızı odasında ışıl ışıl parıldıyor, Giysisi altınla dokunmuş.
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
İşlemeli giysiler içinde kralın önüne çıkarılacak, Arkadaşları, ona eşlik eden kızlar sana getirilecek.
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
Sevinç ve coşkuyla götürülecek, Kralın sarayına girecekler.
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
Atalarının yerini oğulların alacak, Onları önder yapacaksın bütün ülkeye.
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
Adını kuşaklar boyunca yaşatacağım, Böylece halklar sonsuza dek övecek seni.