< Zaburi 45 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
برای رهبر سرایندگان: در مایۀ «سوسنها». قصیدۀ پسران قورَح. ترانۀ عاشقانه. در حالی که این سرود را برای پادشاه می‌سرایم، کلماتی زیبا فکرم را پر می‌سازند. همچون قلمی در دست شاعری توانا، زبانم آماده سرودن است.
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
تو از همهٔ انسانها زیباتری؛ از لبانت نعمت و فیض می‌چکد. خداوند تو را تا ابد متبارک ساخته است.
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
ای دلاور، شمشیر جلال و جبروتت را بر کمر خویش ببند و شکوهمندانه بر اسب خویش سوار شو
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
تا از حقیقت و عدالت و تواضع دفاع کنی. قدرت بازوی تو پیروزی بزرگی را نصیب تو می‌گرداند.
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
تیرهای تیز تو به قلب دشمنانت فرو می‌روند؛ و قومها در برابر تو سقوط می‌کنند.
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
ای خدا، سلطنت تو تا ابد برقرار است؛ اساس حکومت تو، بر عدل و راستی است.
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
عدالت را دوست داری و از شرارت بیزاری؛ بنابراین، خدا، یعنی خدای تو، تو را بیش از هر کس دیگر به روغن شادمانی مسح کرده است.
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
همهٔ لباسهایت به بوی خوش مُر و عود و سلیخه آمیخته است؛ در کاخ عاج تو، نوای موسیقی گوشهایت را نوازش می‌دهد.
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
ندیمه‌های دربارت، شاهزادگانند؛ در سمت راست تو، ملکه با لباس مزین به طلای خالص، ایستاده است.
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
ای دختر، به نصیحت من گوش کن. قوم و خویش و زادگاه خود را فراموش کن
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
تا پادشاه شیفتهٔ زیبایی تو شود. او را اطاعت کن، زیرا او سَروَر توست.
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
اهالی سرزمین صور با هدایا نزد تو خواهند آمد و ثروتمندان قوم تو طالب رضامندی تو خواهند بود.
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
عروسِ پادشاه را نگاه کنید! او در درون کاخش چه زیباست! لباسهایش زربافت می‌باشد.
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
او را با لباس نقشدارش نزد پادشاه می‌آورند؛ ندیمه‌هایش نیز از پی او می‌آیند.
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
آنان با خوشی و شادمانی به درون کاخ پادشاه هدایت می‌شوند.
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
ای پادشاه، تو صاحب پسران بسیار خواهی شد و آنها نیز مانند اجدادت تاج شاهی را بر سر خواهند نهاد، و تو ایشان را در سراسر جهان به حکمرانی خواهی گماشت.
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
نام تو را در تمام نسلها شهرت خواهم داد، و همهٔ مردم تا ابد سپاسگزار تو خواهند بود.

< Zaburi 45 >