< Zaburi 45 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
למנצח על ששנים לבני קרח משכיל שיר ידידת רחש לבי דבר טוב אמר אני מעשי למלך לשוני עט סופר מהיר׃
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
יפיפית מבני אדם הוצק חן בשפתותיך על כן ברכך אלהים לעולם׃
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
חגור חרבך על ירך גבור הודך והדרך׃
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
והדרך צלח רכב על דבר אמת וענוה צדק ותורך נוראות ימינך׃
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
חציך שנונים עמים תחתיך יפלו בלב אויבי המלך׃
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
כסאך אלהים עולם ועד שבט מישר שבט מלכותך׃
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
אהבת צדק ותשנא רשע על כן משחך אלהים אלהיך שמן ששון מחבריך׃
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
מר ואהלות קציעות כל בגדתיך מן היכלי שן מני שמחוך׃
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
בנות מלכים ביקרותיך נצבה שגל לימינך בכתם אופיר׃
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
שמעי בת וראי והטי אזנך ושכחי עמך ובית אביך׃
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
ויתאו המלך יפיך כי הוא אדניך והשתחוי לו׃
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
ובת צר במנחה פניך יחלו עשירי עם׃
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
כל כבודה בת מלך פנימה ממשבצות זהב לבושה׃
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
לרקמות תובל למלך בתולות אחריה רעותיה מובאות לך׃
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
תובלנה בשמחת וגיל תבאינה בהיכל מלך׃
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
תחת אבתיך יהיו בניך תשיתמו לשרים בכל הארץ׃
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
אזכירה שמך בכל דר ודר על כן עמים יהודך לעלם ועד׃

< Zaburi 45 >