< Zaburi 45 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
Jusqu'à la Fin, avec chants alternés, une instruction des fils de Koré, un cantique au sujet du bien-aimé. Mon cœur a exhalé une bonne parole; je dédie mes œuvres au Roi. Ma langue est le roseau d'un scribe écrivant avec rapidité.
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
Tu es plus beau que les fils des hommes; la grâce est répandue sur tes lèvres. A cause de cela, Dieu t'a béni à jamais.
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
Ceins l'épée qui s'appuie sur ta cuisse, ô Puissant!
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
En ta jeunesse et en ta beauté, tends ton arc, marche et prospère, et règne par l'amour de la vérité, de la douceur et de la justice, et ta droite te guidera merveilleusement.
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
Tes traits sont aiguisés, ô Puissant; ils renverseront les peuples; ils perceront le cœur des ennemis du Roi.
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
Ton trône, ô mon Dieu, sera dans les siècles des siècles; ton sceptre de roi est le sceptre de la justice.
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
Tu aimes la justice et tu hais l'iniquité; à cause de cela, ô Dieu, ton Dieu a fait de toi son Christ; il a répondu sur toi plus que sur tes compagnons l'huile de l'allégresse.
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
La myrrhe, les essences et la casse s'exhalent de tes vêtements et de tes palais d'ivoire, et, réunies en ton honneur, elles te réjouissent,
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
Les filles des rois. La reine s'est placée à ta droite, revêtue d'un manteau d'or diversement orné.
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Écoute, ma fille, et vois, et incline ton oreille; oublie ton peuple et la maison de ton père;
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
Car le roi s'est épris de ta beauté, lui qui est ton seigneur:
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
Et les filles de Tyr t'adoreront avec des présents; les riches du peuple de la terre prieront devant ta face.
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
Toute sa gloire est comme celle de la fille du roi d'Esebon, revêtue d'une parure de franges d'or,
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
Et diversement ornée. Les vierges de sa suite sont amenées au roi; ses compagnes te seront amenées.
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
Elles te seront amenées avec joie et allégresse; elles seront conduites en la demeure du Roi.
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
A la place de tes frères, des fils te sont nés; tu les institueras chefs de toute la terre.
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
Ils se souviendront de ton nom de génération en génération; à cause de cela, les peuples te rendront grâces éternellement et dans les siècles des siècles.