< Zaburi 45 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
Au maître de chant. Sur les lis. Cantique des fils de Coré. Chant d’amour. De mon cœur jaillit un beau chant; je dis: « Mon œuvre est pour un roi! » Ma langue est comme le roseau rapide du scribe,
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
Tu es le plus beau des fils de l’homme, la grâce est répandue sur tes lèvres; c’est pourquoi Dieu t’a béni pour toujours.
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
Ceins ton épée sur ta cuisse, ô héros, revêts ta splendeur et ta majesté.
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
Et dans ta majesté avance-toi, monte sur ton char, combats pour la vérité, la douceur et la justice; et que ta droite te fasse accomplir des faits merveilleux.
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
Tes flèches sont aiguës; des peuples tomberont à tes pieds; elles perceront le cœur des ennemis du roi.
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
Ton trône, ô Dieu, est établi pour toujours; le sceptre de ta royauté est un sceptre de droiture.
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
Tu aimes la justice et tu hais l’iniquité: c’est pourquoi Dieu, ton Dieu, t’a oint d’une huile d’allégresse, de préférence à tes compagnons.
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
La myrrhe, l’aloès et la casse s’exhalent de tous tes vêtements; des palais d’ivoire, les lyres te réjouissent.
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
Des filles de rois sont parmi tes bien-aimées; la reine est à ta droite, parée de l’or d’Ophir.
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
« Écoute, ma fille, regarde et prête l’oreille: oublie ton peuple et la maison de ton père,
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
et le roi sera épris de ta beauté; car il est ton Seigneur: rends-lui tes hommages.
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
La fille de Tyr, avec des présents, et les plus riches du peuple rechercheront ta faveur. »
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
Toute resplendissante est la fille du roi dans l’intérieur; son vêtement est fait de tissus d’or.
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
En robe de couleurs variées, elle est présentée au roi; après elles, des jeunes filles ses compagnes, te sont amenées.
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
On les introduit au milieu des réjouissances et de l’allégresse; elles entrent dans le palais du Roi.
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
Tes enfants prendront la place de tes pères; tu les établiras princes sur toute la terre.
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
Je rappellerai ton nom dans tous les âges; et les peuples te loueront éternellement et à jamais.