< Zaburi 45 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
Veisuunjohtajalle; veisataan kuin: "Liljat"; koorahilaisten mietevirsi; laulu rakkaudesta. Minun sydämeni tulvii ihania sanoja; minä lausun: kuninkaasta on minun lauluni, minun kieleni on kerkeän kirjurin kynä.
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
Sinä olet ihmislapsista ihanin, suloisuus on vuodatettu sinun huulillesi, sentähden Jumala siunaa sinua iankaikkisesti.
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
Vyötä miekka vyöllesi, sinä sankari, vyöttäydy kunniaasi ja korkeuteesi.
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
Ole onnekas korkeudessasi. Nouse sotavaunuihisi totuuden, nöyryyden ja vanhurskauden puolesta, ja oikea kätesi opettakoon sinulle peljättäviä tekoja.
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
Sinun nuolesi ovat terävät, kansat kaatuvat sinun allesi; kuninkaan vihollisten sydämet lävistetään.
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
Jumala, sinun valtaistuimesi pysyy aina ja iankaikkisesti; sinun valtakuntasi valtikka on oikeuden valtikka.
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
Sinä rakastat vanhurskautta ja vihaat vääryyttä; sentähden on Jumala, sinun Jumalasi, voidellut sinua iloöljyllä enemmän kuin sinun osaveljiäsi.
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
Mirhaa, aloeta ja kassiaa tuoksuvat kaikki sinun vaatteesi, kanteleet helisevät sinun iloksesi norsunluisista palatseista.
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
Kuningasten tyttäriä on sinun kaunistuksenasi, kuningatar seisoo sinun oikealla puolellasi, Oofirin kullassa.
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Kuule, tytär, katso ja kallista korvasi, unhota kansasi ja isäsi huone,
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
ja saakoon kuningas halun sinun kauneuteesi, sillä hän on sinun herrasi. Kumarra häntä.
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
Tytär Tyyro ja kansan rikkaimmat etsivät lahjoillaan sinun suosiotasi.
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
Ylen ihana on kuninkaan tytär sisäkammiossa, kultakudosta on hänen pukunsa.
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
Kirjailluissa vaatteissa hänet saatetaan kuninkaan tykö. Neitsyet seuraavat häntä, hänen ystävättärensä tuodaan sinun tykösi.
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
Ilolla ja riemulla heitä saatetaan, he astuvat kuninkaan palatsiin.
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
Sinun poikasi tulkoot sinun isiesi sijaan; aseta heidät ruhtinaiksi kaikkeen maahan.
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
Minä teen sinun nimesi kuuluksi suvusta sukuun; sentähden kansat sinua ylistävät aina ja iankaikkisesti.

< Zaburi 45 >