< Zaburi 45 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
For the leader; on shoshannim. Of the Korahites. A maskil. A love song. My heart is astir with beautiful words: I will sing a song, concerning the king, with tongue like the pen of a ready writer.
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
Your beauty is more than mortal, grace is shed over your lips: therefore God has blessed you forever.
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
Warrior, strap your sword on your thigh. What glory and splendor!
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
Good fortune attend you, as forth you ride in the cause of good faith, and as champion of justice. May your arm instruct you in deeds of dread.
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
Sharp are your arrows; nations fall under you: pierced to the heart are the foes of the king.
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
Your throne shall endure for ever and ever your royal sceptre a sceptre of equity.
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
Right you love and wrong you hate: therefore the Lord your God anoints you With oil of gladness above your fellows.
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
With myrrh, aloes, and cassia your robes are all fragrant, you are gladdened by music of ivory harps.
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
King’s daughters stand ready with jewels for you, at your right hand the queen in gold of Ophir.
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Listen, daughter, and see; and incline your ear: forget your folk and your father’s house.
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
And when the king desires your beauty, bow to him, for he is your lord.
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
So shall the Tyrians come with gifts, and the richest of people will do you homage.
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
The king’s daughter is glorious altogether, with dress of pearls inwrought with gold.
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
In many-coloured robes she is led to the king, with the virgin companions she brought in her train.
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
The king’s palace they enter with joy and rejoicing.
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
May sons of yours take the place of your fathers, whom you will make princes in all the land.
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
Your name will I celebrate world without end, so that nations shall praise you for ever and ever.

< Zaburi 45 >