< Zaburi 45 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
For the end, for alternate [strains] by the sons of Core; for instruction, a Song concerning the beloved. My heart has uttered a good matter: I declare my works to the king: my tongue is the pen of a quick writer.
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
Thou art more beautiful than the sons of men: grace has been shed forth on thy lips: therefore God has blessed thee for ever.
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
Gird thy sword upon thy thigh, O Mighty One, in thy comeliness, and in thy beauty;
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
and bend [thy bow], and prosper, and reign, because of truth and meekness and righteousness; and thy right hand shall guide thee wonderfully.
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
Thy weapons are sharpened, Mighty One, (the nations shall fall under thee) [they are] in the heart of the king's enemies.
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
Thy throne, O God, is for ever and ever: the sceptre of thy kingdom is a sceptre of righteousness.
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
Thou hast loved righteousness, and hated iniquity: therefore God, thy God, has anointed thee with the oil of gladness beyond thy fellows.
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
Myrrh, and stacte, and cassia [are exhaled] from thy garments, [and] out of the ivory palaces,
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
with which kings' daughters have gladdened thee for thine honour: the queen stood by on thy right hand, clothed in vesture wrought with gold, [and] arrayed in divers colours.
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Hear, O daughter, and see, and incline thine ear; forget also thy people, and thy father's house.
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
Because the king has desired thy beauty; for he is thy Lord.
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
And the daughter of Tyre shall adore him with gifts; the rich of the people of the land shall supplicate thy favour.
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
All her glory [is that] of the daughter of the king of Esebon, robed [as she is] in golden fringed garments,
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
in embroidered [clothing]: virgins shall be brought to the king after her: her fellows shall be brought to thee.
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
They shall be brought with gladness and exultation: they shall be led into the king's temple.
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
Instead of thy fathers children are born to thee: thou shalt make them princes over all the earth.
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
They shall make mention of thy name from generation to generation: therefore shall the nations give thanks to thee for ever, even for ever and ever.