< Zaburi 45 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
To the chief music-maker; put to Shoshannim. Of the sons of Korah. Maschil. A Song of loves. My heart is flowing over with good things; my words are of that which I have made for a king; my tongue is the pen of a ready writer.
2 Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
You are fairer than the children of men; grace is flowing through your lips; for this cause the blessing of God is with you for ever.
3 Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
Put on your sword, make it ready at your side, O strong chief, with your glory and power.
4 Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
And go nobly on in your power, because you are good and true and without pride; and your right hand will be teaching you things of fear.
5 Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
Your arrows are sharp in the heart of the king's haters; because of them the peoples are falling under you.
6 Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
Your seat of power, O God, is for ever and ever; the rod of your kingdom is a rod of honour.
7 Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
You have been a lover of righteousness and a hater of evil: and so God, your God, has put the oil of joy on your head, lifting you high over all other kings.
8 Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
Your robes are full of the smell of all sorts of perfumes and spices; music from the king's ivory houses has made you glad.
9 Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
Kings' daughters are among your noble women: on your right is the queen in gold of Ophir.
10 Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
O daughter, give thought and attention, and let your ear be open; no longer keep in mind your people, and your father's house;
11 Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
So will the king have a great desire for you, seeing how beautiful you are; because he is your lord, give him honour.
12 Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
And the daughters of Tyre will be there with an offering; those who have wealth among the people will be looking for your approval.
13 Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
In the great house the king's daughter is all shining: her clothing is worked with gold.
14 Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
She will come before the king in robes of needlework; the virgins in her train will come before you.
15 Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
With joy and rapture will they come; they will go into the king's house.
16 Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
Your children will take the place of your fathers; so that you may make them rulers over all the earth.
17 Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.
I will keep the memory of your name living through all generations; and because of this the people will give you praise for ever.

< Zaburi 45 >