< Zaburi 42 >
1 Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora. Kama vile ayala aoneavyo shauku vijito vya maji, ndivyo nafsi yangu ikuoneavyo shauku, Ee Mungu.
Načelniku godbe med nasledniki Koretovimi; ukovita. Kakor jelen koprni po vodnih potokih, tako duša moja koprni po tebi, Bog.
2 Nafsi yangu inamwonea Mungu kiu, Mungu aliye hai. Ni lini nitaweza kwenda kukutana na Mungu?
Žejna je duša moja Boga, mogočnega, živega, govoreč: Kdaj se približam, da se prikažem pred obličjem Božjim?
3 Machozi yangu yamekuwa chakula changu usiku na mchana, huku watu wakiniambia mchana kutwa, “Yuko wapi Mungu wako?”
Solzé moje so mi za hrano podnevi in ponoči; ko se mi pravi vsak dan: Kje je, tvoj Bog?
4 Mambo haya nayakumbuka ninapoimimina nafsi yangu: Jinsi nilivyokuwa nikienda na umati wa watu, nikiongoza maandamano kuelekea kwenye nyumba ya Mungu, kwa kelele za shangwe na za shukrani katikati ya umati uliosherehekea.
To mi je v mislih, ko izlivam v sebi dušo svojo, da bi se bil izprehajal v krdelu, hodil z njimi noter do hiše Božje z glasom petja in hvale, v praznični množici.
5 Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka? Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu? Weka tumaini lako kwa Mungu, kwa sababu bado nitamsifu, Mwokozi wangu na
Kaj si pobita, duša moja, in tako ropočeš v meni? Upaj v Boga, ker še ga bodem slavil in vso blaginjo njegovega obličja.
6 Mungu wangu. Nafsi yangu inasononeka ndani yangu; kwa hiyo nitakukumbuka kutoka nchi ya Yordani, katika vilele vya Hermoni, kutoka Mlima Mizari.
Bog moj, pobita je v meni duša moja; zatorej se spominjam tebe iz dežele Jordanove in Hermonske, z male gorice.
7 Kilindi huita kilindi, katika ngurumo za maporomoko ya maji yako; mawimbi yako yote pamoja na viwimbi vimepita juu yangu.
Brezno kliče brezno o slapov tvojih glasu; vse vodé tvoje in valovi tvoji pridirajo in valé se čez me.
8 Mchana Bwana huelekeza upendo wake, usiku wimbo wake uko nami: maombi kwa Mungu wa uzima wangu.
Podnevi pošlje Gospod milost svojo, in ponoči hvalno pesem svojo k meni; v molitvi svoji k Bogu mogočnemu življenja mojega prebijem.
9 Ninamwambia Mungu Mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini niendelee kuomboleza, nikiwa nimeonewa na adui?”
Govoril bodem Bogu mogočnemu, skali svoji: Zakaj me pozabljaš? zakaj hodim žalujoč zaradi zatiranja sovražnikovega?
10 Mifupa yangu inateseka kwa maumivu makali adui zangu wanaponidhihaki, wakiniambia mchana kutwa, “Yuko wapi Mungu wako?”
Suhe kosti moje napadajo, sramoté me sovražniki moji, govoré mi vsak dan: Kje Bog je tvoj?
11 Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka? Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu? Weka tumaini lako kwa Mungu, kwa sababu bado nitamsifu, Mwokozi wangu na Mungu wangu.
Kaj si pobita, duša moja, in kaj tako ropočeš v meni? Upaj v Boga, ker še ga bodem slavil, vso blaginjo obličja mojega in mojega Boga.