< Zaburi 41 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
Al Músico principal: Salmo de David. BIENAVENTURADO el que piensa en el pobre: en el día malo lo librará Jehová.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
Jehová lo guarde, y le dé vida: sea bienaventurado en la tierra, y no lo entregues á la voluntad de sus enemigos.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
Jehová lo sustentará sobre el lecho del dolor: mullirás toda su cama en su enfermedad.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
Yo dije: Jehová, ten misericordia de mí; sana mi alma, porque contra ti he pecado.
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
Mis enemigos dicen mal de mí [preguntando]: ¿Cuándo morirá, y perecerá su nombre?
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
Y si venía á ver[me], hablaba mentira: su corazón se amontonaba iniquidad; y salido fuera, hablába[la].
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
Reunidos murmuraban contra mí todos los que me aborrecían: contra mí pensaban mal, [diciendo de mí]:
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
Cosa pestilencial de él se ha apoderado; y el que cayó en cama, no volverá á levantarse.
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Aun el hombre de mi paz, en quien yo confiaba, el que de mi pan comía, alzó contra mí el calcañar.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
Mas tú, Jehová, ten misericordia de mí, y hazme levantar, y daréles el pago.
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
En esto habré conocido que te he agradado, que mi enemigo no se holgará de mí.
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
En cuanto á mí, en mi integridad me has sustentado, y me has hecho estar delante de ti para siempre.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Bendito sea Jehová, el Dios de Israel, por siglos de siglos. Amén y Amén.

< Zaburi 41 >