< Zaburi 41 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
Para el músico principal. Un salmo de David. Dichoso el que considera a los pobres. Yahvé lo librará en el día del mal.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
Yahvé lo preservará y lo mantendrá con vida. Será bendecido en la tierra, y no lo entregará a la voluntad de sus enemigos.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
Yahvé lo sostendrá en su lecho de enfermo, y restaurarlo de su lecho de enfermedad.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
Dije: “¡Yahvé, ten piedad de mí! Cúrame, porque he pecado contra ti”.
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
Mis enemigos hablan mal de mí: “¿Cuándo morirá y perecerá su nombre?”
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
Si viene a verme, habla con falsedad. Su corazón recoge la iniquidad para sí mismo. Cuando va al extranjero, lo cuenta.
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
Todos los que me odian susurran juntos contra mí. Se imaginan lo peor para mí.
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
“Una mala enfermedad”, dicen, “lo ha afligido. Ahora que yace no se levantará más”.
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Sí, mi propio amigo familiar, en quien confié, que comió el pan conmigo, ha levantado su talón contra mí.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
Pero tú, Yahvé, ten piedad de mí y levántame, para que yo les pague.
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
Por esto sé que te deleitas en mí, porque mi enemigo no triunfa sobre mí.
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
En cuanto a mí, me sostienes en mi integridad, y ponme en tu presencia para siempre.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Benditosea Yahvé, el Dios de Israel, ¡desde la eternidad y hasta la eternidad! Amén y amén.