< Zaburi 41 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
In finem, Psalmus ipsi David. Beatus qui intelligit super egenum, et pauperem: in die mala liberabit eum Dominus.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
Dominus conservet eum, et vivificet eum, et beatum faciat eum in terra: et non tradat eum in animam inimicorum eius.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
Dominus opem ferat illi super lectum doloris eius: universum stratum eius versasti in infirmitate eius.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
Ego dixi: Domine miserere mei: sana animam meam, quia peccavi tibi.
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
Inimici mei dixerunt mala mihi: Quando morietur, et peribit nomen eius?
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
Et si ingrediebatur ut videret, vana loquebatur, cor eius congregavit iniquitatem sibi. Egrediebatur foras, et loquebatur
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
in idipsum. Adversum me susurrabant omnes inimici mei: adversum me cogitabant mala mihi.
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
Verbum iniquum constituerunt adversum me: Numquid qui dormit non adiiciet ut resurgat?
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Etenim homo pacis meæ, in quo speravi: qui edebat panes meos, magnificavit super me supplantationem.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
Tu autem Domine miserere mei, et resuscita me: et retribuam eis.
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
In hoc cognovi quoniam voluisti me: quoniam non gaudebit inimicus meus super me.
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
Me autem propter innocentiam suscepisti: et confirmasti me in conspectu tuo in æternum.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Benedictus Dominus Deus Israel a sæculo, et usque in sæculum: fiat, fiat.

< Zaburi 41 >