< Zaburi 41 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
Al maestro del coro. Salmo. Di Davide. Beato l'uomo che ha cura del debole, nel giorno della sventura il Signore lo libera.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
Veglierà su di lui il Signore, lo farà vivere beato sulla terra, non lo abbandonerà alle brame dei nemici.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
Il Signore lo sosterrà sul letto del dolore; gli darai sollievo nella sua malattia.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
Io ho detto: «Pietà di me, Signore; risanami, contro di te ho peccato».
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
I nemici mi augurano il male: «Quando morirà e perirà il suo nome?».
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
Chi viene a visitarmi dice il falso, il suo cuore accumula malizia e uscito fuori sparla.
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
Contro di me sussurrano insieme i miei nemici, contro di me pensano il male:
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
«Un morbo maligno su di lui si è abbattuto, da dove si è steso non potrà rialzarsi».
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Anche l'amico in cui confidavo, anche lui, che mangiava il mio pane, alza contro di me il suo calcagno.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
Ma tu, Signore, abbi pietà e sollevami, che io li possa ripagare.
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
Da questo saprò che tu mi ami se non trionfa su di me il mio nemico;
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
per la mia integrità tu mi sostieni, mi fai stare alla tua presenza per sempre.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Sia benedetto il Signore, Dio d'Israele, da sempre e per sempre. Amen, amen.