< Zaburi 41 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
Au chef des chantres. Psaume de David. Heureux celui qui s’intéresse au pauvre! Au jour de la calamité, l’Eternel le sauvera.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
L’Eternel le protégera, lui conservera la vie, et il jouira du bonheur sur la terre: tu ne le livreras pas à la fureur de ses ennemis.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
Le Seigneur le soutiendra sur le lit de douleur; sa couche, tu la retournes entièrement dans sa maladie.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
Je dis donc, moi: "Eternel, sois-moi propice! Guéris mon âme, car j’ai péché contre toi."
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
Mes ennemis tiennent de méchants propos à mon sujet: "Quand mourra-t-il pour que son nom périsse?"
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
Que si l’un d’eux vient me voir, son cœur exprime des faussetés et fait une provision de méchanceté: il me quitte pour sortir et la débiter.
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
Ensemble, tous mes adversaires chuchotent contre moi; contre moi, ils imaginent de funestes pensées:
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
"Un mauvais sort s’acharne après lui; dès lors qu’il est couché, il ne se relèvera plus!"
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Même mon ami intime, en qui j’avais confiance, et qui mangeait mon pain, a levé le talon contre moi.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
Or donc, Eternel, prends-moi en pitié et relève-moi, pour que je puisse leur rendre la pareille.
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
A cela je reconnaîtrai que tu m’as pris en affection: que mon ennemi ne triomphe pas de moi!
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
En raison de mon intégrité, tu me soutiens et m’admets en ta présence pour toujours.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Loué soit l’Eternel, Dieu d’Israël, d’éternité en éternité! Amen et Amen!

< Zaburi 41 >