< Zaburi 41 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
For victorie, the song of Dauid. Blessid is he that vndurstondith `on a nedi man and pore; the Lord schal delyuere hym in the yuel dai.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
The Lord kepe hym, and quykene hym, and make hym blesful in the lond; and bitake not hym in to the wille of his enemyes.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
The Lord bere help to hym on the bed of his sorewe; thou hast ofte turned al his bed stre in his sijknesse.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
I seide, Lord, haue thou mercy on me; heele thou my soule, for Y synnede ayens thee.
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
Myn enemyes seiden yuels to me; Whanne schal he die, and his name schal perische?
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
And if he entride for to se, he spak veyn thingis; his herte gaderide wickidnesse to hym silf.
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
He yede with out forth; and spak to the same thing. Alle myn enemyes bacbitiden pryuyli ayens me; ayens me thei thouyten yuels to me.
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
Thei ordeineden an yuel word ayens me; Whether he that slepith, schal not leie to, that he rise ayen?
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
For whi the man of my pees, in whom Y hopide, he that eet my looues; made greet disseit on me.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
But thou, Lord, haue merci on me, and reise me ayen; and Y schal yelde to hem.
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
In this thing Y knew, that thou woldist me; for myn enemye schal not haue ioye on me.
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
Forsothe thou hast take me vp for ynnocence; and hast confermed me in thi siyt with outen ende.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Blessid be the Lord God of Israel, fro the world and in to the world; be it doon, be it doon.

< Zaburi 41 >