< Zaburi 41 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
To the chief Musician, A Psalm of David. Blessed [is] he that considereth the poor: the LORD will deliver him in the time of trouble.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
The LORD will preserve him, and keep him alive; [and] he shall be blessed upon the earth: and thou wilt not deliver him to the will of his enemies.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
The LORD will strengthen him upon the bed of languishing: thou wilt make all his bed in his sickness.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
I said, LORD, be merciful to me: heal my soul; for I have sinned against thee.
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
My enemies speak evil of me, When shall he die, and his name perish?
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
And if he cometh to see [me], he speaketh vanity: his heart gathereth iniquity to itself; [when] he goeth abroad, he telleth [it].
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
All that hate me whisper together against me: against me do they devise my hurt.
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
An evil disease, [say they], cleaveth fast to him: and [now] that he lieth he shall rise no more.
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Yes, my own familiar friend, in whom I trusted, who ate of my bread, hath lifted up [his] heel against me.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
But thou, O LORD, be merciful to me, and raise me up, that I may requite them.
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
By this I know that thou favorest me, because my enemy doth not triumph over me.
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
And as for me, thou upholdest me in my integrity, and settest me before thy face for ever.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Blessed [be] the LORD God of Israel from everlasting, and to everlasting. Amen, and amen.

< Zaburi 41 >