< Zaburi 41 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
Yahweh is pleased with those people who help to provide for the poor; he will rescue those people when they have troubles.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
Yahweh protects them and allows them to live [for a long time]. He enables them to be happy in the land [of Israel], and rescues them from their enemies.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
When they are sick, Yahweh strengthens them, and he heals them.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
[When I was sick], I said, “Yahweh, be merciful to me and heal me; [I know that I am sick because] I have sinned against you.”
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
My enemies say cruel things about me; they say, “How soon will he die, and then everyone will forget about him [MTY]? (OR, he will not have [any descendants to continue] his name).”
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
When my enemies come to me, they falsely say that they [are concerned about me]. They listen to bad news about (me/my health). Then they go away and tell everywhere what is happening to me.
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
All those who hate me whisper to others about me, and they hope/desire that very bad things will happen to me.
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
They say, “He will soon die because of his being sick; he will never get up from his bed [before he dies].”
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Even my best friend, whom I trusted very much, who [often] ate with me, has (betrayed me/put me into my enemies’ hands) [IDM].
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
But Yahweh, be merciful to me, and enable me to become healthy [again]. When you do that, I will be able to (pay back my enemies/get revenge on my enemies/cause my enemies to suffer like they caused me to suffer).
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
[If you enable me to] do that, with the result that my enemies do not defeat me, I will know that you are pleased with me.
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
[I will know that] it is because I have done what is right that you have helped me, and [I will know that] you will let me be with you forever.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Praise Yahweh, the God whom we Israelis [worship]; Praise him forever! Amen! I desire that it will be so!