< Zaburi 41 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
“For the leader of the music. A psalm of David.” Happy is he who hath regard to the poor! The LORD will deliver him in time of trouble.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
The LORD will preserve him, and keep him alive; He shall be happy on the earth; Thou wilt not give him up to the will of his enemies!
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
The LORD will strengthen him upon the bed of disease; All his bed thou wilt change in his sickness.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
I said, O LORD! be merciful to me! Heal me, for I have sinned against thee!
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
My enemies speak evil of me: “When will he die, and his name perish?”
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
If one come to see me, he speaketh falsehood; His heart gathereth malice; When he goeth abroad, he uttereth it.
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
All that hate me whisper together against me; Against me do they devise mischief:
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
“A deadly disease cleaveth fast unto him; He lieth down, and he shall never arise!”
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Yea, my familiar friend in whom I trusted, who did eat of my bread, —He hath lifted up his heel against me.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
But do thou, O LORD! have pity upon me; Raise me up, that I may requite them!
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
By this I know that thou favorest me, Because my enemy doth not triumph over me.
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
As for me, thou wilt uphold me in my integrity; Thou wilt set me before thy face for ever!
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
[Praised be Jehovah, the God of Israel, From everlasting to everlasting. Amen! Amen!]

< Zaburi 41 >